Skip to main content

JINSI YA KUANDIKA BARUA YA KIKAZI


JINSI YA KUANDIKA BARUA YA KIKAZI

Utajifunza
  • Lengo la kuandika barua ya kikazi
  • Ukubwa wa barua yako?
  • Jinsi ya kulinganisha barua yako iendane na kazi unayoomba
  • Nini kinatakiwa kwenye barua yako
  • Kipi kisichotakiwa kwenye barua yako
  • Aina tofauti ya barua za kikazi
Pia Makala hii itakuonyesha:
  • Jinsi ya kuandika barua bora yenye asilimia 9 kati ya 10.
  • Utaona mfano wa barua ambao utapelekea kuitwa kwenye Usahili/interviews (na kwanini).
  • Utajifunza mbinu mbalimbali za kuandika barua itakayopelekea upate kazi kiurahisi
  • Utajifunza jinsi ya kuanza naa kumaliza barua yako na jinsi ya kuiwasilisha.

Barua ya kikazi ni barua inayoandikwa kwa ukurasa mmoja ambayo inaambatanishwa wakati wa maombi ya kazi.

KUSUDI LA KUANDIKA BARUA YA KIKAZI
Wakati unaandika barua, unatakiwa:
  • kujitambulisha
  • Orodhesha kazi unayotaka kuomba
  • Onyesha ujuzi na uzoefu wako kuwa vinaendana na kazi unayoomba.
  • Mshawishi msomaji aendelee kusoma na CV yako
Barua ya kikazi inatakiwa iwe na urefu gani?
Ifanye iwe fupi. Barua ni ufupisho wa CV yako kwaiyo usiandike zaidi ya ukurasa mmoja.

Linganisha barua yako iendane na kazi unayoomba.
Tumia barua tofauti kwa kila kazi unayoomba, barua yako inatakiwa ionyeshe unaijua kazi unayoiomba. Na kipi mwajiri anataka kukiona
Kwa kufanya hivi, Onyesha ujuzi na ubora wako ambao unaendana na mahitaji ya kazi unayoomba.

1. Tafuta mtu sahihi ambaye anapaswa kuandikiwa barua.
Mara nyingi kwenye matangazo ya kazi huwa wanaandika mtu anayepaswa kuandikiwa barua. Likini kuna baadhi ya barua ambazo unatakiwa uwandike bila ya kuona Tangazo unapaswa utafute mtu sahihi ambaye atasoma na kuifanyia kazi barua yako.

2. Tafuta zaidi maelezo ya kutosha kuhusiana na kazi hiyo

3. Tafuta maelezo zaidi ya kuhusu Kampuni unayoomba kazi
  • Kama unajua jina la kampuni unayoomba kazi tafuta maelezo yake mtandaoni au jaribu kuuliza watu
  • Kama kampuni ina tovuti ingia na uangalie sehemu ya About/Kuhusu na usome kwa makini kampuni au taasisi inajishughulisha na nini.
Kipi kinatakiwa kuwepo kwenye barua yako
Hivi ni vitu vinavyotakiwa kwenye barua yako ya kikazi

Jina lako, Anuani yako na mawasiliano yako.
Andika jina, anuani na mawasiliano yako juu kabisa ya barua yako. Haitoshi tu kuweka anuani yako pekee ila weka na email na namba za simu.

Anuani ya kampuni au jina la mtu inayemfikia
Hakikisha unaandika anuani sahihi kwa mtu sahihi.

Jina la kazi unayoomba.
Mwanzo wa barua unatakiwa uandike kazi unayoomba hasa kwenye kichwa cha barua.
Pia unaweza ukaandika mwanzo wa aya ya kwanza.

Orodhesha ujuzi wako unafanana na Ajira au kazi unayoomba.
Eleza kwa ufupi kuhusu ujuzi wako unaoendana na kazi unayoomba.
Kumbuka kuwa kama unasema una ujuzi unatakiwa useme jinsi utakavoutumia iwapo utapata kazi hiyo na kama ulishawahi kuutumia huo ujuzi.

Andika kwanini wewe unafaa zaidi kwa kazi hiyo.
Baada ya kuorothesha ujuzi wako unatakiwa uelezee kwanini wewe unafaa zaidi kwa kazi hiyo, kipi kitu cha pekee ambacho unacho kitakachowavutia waajiri wako ili wakuajiri.

Waombe  waajiri wako wakutafute
Barua yako lazima imalize kwa kuomba waajiri wako wasome CV yako pia waombe wafanye mawasiliano na wewe.
Mfano nimeambatanisha na CV yangu, ni mategemeo yangu nitasikia chochote kutoka kwenu.

Kipi kinatakiwa kisiwepo kwenye barua yako ya kikazi.
Kuna vitu ambavyo havitakiwi kuwepo katika barua yako ya kikazi.

Kukosea baadhi ya maneno
Makosa ya kimaandishi kwenye barua yako kama kukosea baadhi ya maneno au kuunganisha maneno.
Hakiki barua yako zaidi ya mara mbili kabla haujaituma kama umeandika jina la kampuni hakikisha umeandika kwa usahihi, kama sehemu au eneo hakikisha umeandika kwa usahihi.

Kuambatanisha CV yako yote kwenye barua
Usi kopi na kuweka CV yako yote kwenye barua yako ya kikazi. Kumbuka barua yako ni ufupisho wa kile kilichopo kwenye CV.

Matumizi ya mimi yaliyozidi
Jaribu kutokutumia maneno kama mimi ninaamini, mimi nina, mimi nip, hapa siyo. Kumbuka hapa siyo kuhusu wewe ila ni kujielezea ni jinsi gani unaweza kumsaidia muajiri ili atimize malengo yake iwapo atakuchagua wewe kuwa mfanyakazi wake.
Baada ya kuandika barua yako jitahidi kuipitia tena na jaribu kuondoa sentensi zote zilizojaa neon la mimi.

Epuka kutaja maombi yako ya kazi nyingine.
Kiukweli huwa tunaomba kazi zaidi ya moja ni vizuri kutokueleza kuwa umeomba na kazi nyingine kwa watu wengine inayoendana na hiyo, lengo letu ni kumshawishi muajiri kuwa una uchu na ukwasi wa kazi hiyo.

Aina tofauti ya Barua za kikazi
  • Barua ya kikazi ambayo hauna ujuzi wowote (fresh from school)
  • Barua ya kikazi ambayo tayari una ujuzi (ulishafanya kazi sehemu)
  • Barua ya kikazi ambayo CV haihitajiki
  • Barua ya kikazi ambayo haina Tangazo.

KWA MAHITAJI YA BARUA ZA KIKAZI 
MUONGOZO/SAMPLE 300/=
KUANDIKIWA BARUA NZIMA 500/= 


Comments